Subscribe Us

header ads

FAIDA ZA UKWAJU KIAFYA NA UREMBO

 


 

Ili uwe wa kwanza kupata machapisho yetu kila siku usisahau kubonyeza button  ya follow  kulike na kukoment . na kama unaswali zaid ruhusa kuuliza kupitia kiboksi hapo chini  . ahsaante

Faida 6 Za Ukwaju Katika Urembo,Afya Na Nywele 

Wengi wetu ni wapenzi wa juice ya hili tunda na wengi tunaitumia majumbani kupunguza uzito, lakini kumbe ukwaju una matumizi mengi tofauti tofauti ukianzia kwenye afya, urembo na hata nywele.

Katika Ngozi husaidia

Katika Nywele husaidia

  • Kuzuia Kukatika Kwa Nywele
  • Husaidia kutibu ngozi ya kichwa yenye mafuta

Katika Afya Ukwaju

  • unasaidia kupunguza uzito

Jinsi ambavyo unaweza kutumia ukwaju kwa ajili ya ngozi

kungarisha ngozi 

mahitaji

  • tunda za ukwaju – 30 grams ( robo kilo)
  • maji ya moto – 150 grams ( chupa mbili za George weah/drop kubwa)
  • manjano – nusu kijiko cha chai

Namna ya kufanya

  • loweka tunda za ukwaju katika maji ya moto kwa dakika kumi
  • toa mbegu na ubaki na juice nzito ya ukwaju
  • ongeza manjano katika juice hio ya ukwaju\
  • paka mchanganyiko wako katika uso wako na uache kwa dakika 15
  • osha kwa maji ya vuguvugu

Note – mchanganyiko huu unasaidia zaidi kwa wenye sura/nyuso zenye mafuta unaweza kufanya hivi mara mbili kwa week.

Kuondoa weusi kwenye shingo 

Mahitaji

  • juice ya ukwaju nzito – kijiko kimoja
  • asali – kijiko kimoja
  • rose water ( maji ya mawardi)– kijiko kimoja

Namna Ya Kufanya

  • changanya juice ya ukwaju, rose water na asali
  • paka mchanganyiko huu katika shingo na uuache  kwa dakika 20
  • osha shingo yako kwa rose water au maji ya uvuguvugu

Fanya hivi mara moj kwa wiki katika kipindi cha miezi miwili utaona matokeo

Kutibu chunusi

Mahitaji

  • juice ya ukwaju – kijiko kimoja
  • mtindi â€“ kijiko kimoja
  • manjano â€“ kijiko kimoja

Matumizi

  • changanya mahitaji yako ( mtindi, ukwaju na manjano)
  • paka usoni na ukae nao mpaka ukauke, unaweza kuchukua dk 20-30
  • osha uso kwa maji ya vuguvugu na paka mafuta kwa ajili ya ku moisturize ngozi

Fanya hivi mara mbili kwa wiki sio tu itaondoa chunusi bali pia itakupa ngozi nyororo

Ukwaju Katika Nywele

Kuzuia ukatikaji wa nywele  

Mahitaji

  • 15 gram za ukwaju ( ukwaju  robo ugawe mara nne)

Matumizi

  • loweka ukwaju wako katika maji  acha kwa dakika 10
  • toa mbegu na upate juice ya ukwaju, paka katika nywele na ngozi ya nywele massage kwa dakika kadhaa ( si zaid ya 10)
  • tumbukiza taulo katika maji ya moto na ukamue kidogo
  • tumia taulo hili kufunga kichwa chako kikiwa bado kina mchanganyiko huo, acha mchanganyiko huu kwa nusu saa.
  • osha mchanganyiko wako kwa shampoo ukifuatiwa na conditioner

fanya hivi mara mbili kwa week kuzuia kukatika kwa nywele

Husaidia kutibu ngozi ya kichwa yenye mafuta( mba)

ngozi yenye mafuta inaweza kusababisha matatizo mengi kwenye nywele ikiwepo m’ba na kukatika kwa nywele

Mahitaji

  • juice ya ukwaju (nzito) – vijiko viwili
  • olive oil â€“ kijiko kimoja
  • butter milk – kijiko kimoja

Matumizi

  • changanya juice ya ukwaju,olive oil na butter milk
  • paka mchanganyiko wako katika nywele na umassage kwa muda wa dk 5-10
  • acha mchanganyiko wako ukae kwa dakika 15, kama utakua unakukera vaa mfuko wa plastic
  • osha kwa kutumia maji ya vuguvugu  na shampoo

rudia kufanya hivi mara mbili kwa wiki kuondoa mafuta katika ngozi ya nywele zako.

unasaidia kupunguza uzito

Mahitaji 

  • Ukwaju na maji

Matumizi

  • unaweza kutengeneza kama juice ama kuwa una weka ukwaju katika maji yako ya kunywa
  • kutumia kinywaji hichi mara mbili kwa siku unaweza kupungua uzito kwa haraka, masaa matatu baada ya kula na muda wa kulala

Note: Ukwaju una uwezo mkubwa wa kupunguza mwili, usitumie kinywaji hiki kama huna mwili mkubwa sana na kama una vidonda vya tumbo.

Ili uwe wa kwanza kupata machapisho yetu kila siku usisahau kubonyeza button  ya follow  kulike na kukoment . na kama unaswali zaid ruhusa kuuliza kupitia kiboksi hapo chini  . ahsaante

 

 

 


Post a Comment

0 Comments