Subscribe Us

header ads

SABABU ZA BARKA KATIKA NYUMBA

 


SABABU ZA BARKAH KATIKA NYUMBA

‘’Na lau kwamba watu wa mji(nyumba)

wangeamini na kumcha mungu tungeliwafungulia

juu yao Baraka kutoka mbinguni na ardhin’’




1. Bismillah na kumtaja allah

amesema rasulu llah (s.a.w)’’anapoingia mmoja

wenu katika nyumba basi na amtaje allah (s.w)

wakati anapoingia na wakati

anapokula,husema shetwani kumwambia mtu

huyo sitakuja mchana wala usiku’’


2. Kuswali swala kwa wakati

Amesema allah (s.w)’’na uamrishe watu wako

kuswali na wawe na subra nayo hatuta kuuliza

rizki kwani sisi tutakuruzuku na mwisho mwema

kwa wamchao mungu’’.



3. Kusoma qur-an tukufu

Amesema rasulu llah (s.a.w)’’someni surat

bakrah kwani kuisoma kwake ni Baraka na

kuiacha kwake ni khasara na wala

hatoihifadhi mnafiki’’

4.kumcha mungu

Amesema allah (s.w) ‘’ ’Na lau kwamba watu wa

mji(nyumba) wangeamini na kumcha mungu

tungeliwafungulia juu yao Baraka kutoka mbinguni

na ardhin na lakini wamekanusha tukayachukua

waliyokua nayo kwa yale muliyoyachuma kwa

mikono yenu’’


5.kula chakula kwa pamoja

Amesema rasulullah (s.a.w)’’kuleni kwa pamoja na

wala musitengane kwani barka hupatikana kwa

kula pamoja,chakula cha mmoja hutosha

wawili,chakula cha wawili hutosha watatu na

wanne’’



6.kutafuta riski mapema(asubuhi mapema)

Amesema rasulullah(s.a.w)’’barka za ummati

wangu zipo katika kutafuta riski kwa

mapema’’(yaani kutoka mapema kuelekea kutafuta

riski).



7.kumtegemea allah kikweli

Amesema rasulullah(s.a.w)’’ lau kama

mtamtegemea allah kiukweli atakuruzukuni kama

anavyowaruzuku ndege hutoka asubuhi matumbo

matupu na akirudi ameshiba’’

8. kuwa wakweli wakati wa manunuzi na mauzaji

Amesema rasulullah ‘’uzianeni kwa kheir bila kuleta

mtafaruko,kwani ukweli huleta barka katika

mauziano na uongo huondosha barka’’



9.sadaka

Miongoni mwa sababu za barka katika nyumba ni

kutoa sadaka hasa hasa kutoa kwa siri kwani

hupunguza ghadhabu za mungu


10.kuswali kwa pamoja mume na mke kwa upole

Amesema rasulullah’’kwa anaetaka kufunguliwa

riski na aswali kwa upole.’’


11.kushukuru sana kwa kila jambo

Amesema allah(s.w)’’ na lau kama mtanishukuru

basi nitawazidishieni’’


12.kukithirisha sana na kudumu na istighfaru

Amesema rasulullah (s.a.w)’’yeyote ataye dumu na

istighfaru allah atamjalia wepesi kila penye ziki na

humpa faraja kila panapotatizo na humruzuku rizki

bila kipimo’’.

~~~~~~~~~wallah aalamu~~~~~~~~~~

Kitabu hiki ni sadaka kwa ajili ya marehemu baba

yangu na afya njema kwa familia yangu ni ruhusa

kutoa kopi na kueneza kwa waislam wengine kwa

lengo la kupata barka kutoka kwa allah.

Namuomba allah atuwafikishe katika mambo ya

kheir.

please eneza link hii ili wengine iwafikie iwe sadaka kwangu na kwako pia.


Post a Comment

0 Comments