Subscribe Us

header ads

uandishi wa insha


UANDISHI WA INSHA

 TARATIBU ZA UANDISHI
Alama na mpangilio wa maneno ni mojawapo ya vigezo vya kutambulisha mwandishi bora hodari kaziiwezekuwa nzuri inayoeleweka na wasomaji, mwandishi hana budi kutumia mfumo wa alama ili kumsaidia msomaji wapi pa kumpumzisha, kuuliza swali n.k baadhiya alama zifuatazo hutumika katika uandishi.
 Mkato (,)
 Alama hii hutumika
 -  kuweka pumziko fupi katika sentensi
 -  kutenga maneno yaliyo katika orodha
 -  huonyesha sehemu mbili za sentensi zilizo kinyume
 Mfano: - Umoja ni nguvu, utengano ni dhaifu
 NUKTA (.)
 Alama hii hutumika
 -  kukamilisha sentensi
 -  kuonyesha ufupisho wa maneno
 mfano: - R.T.D (Radio Tanzania Dar es salaam)
 NUKTA MKATO (;)
 Alama hii hutumika
 Kuunga sentensi mbili zinazoweza kusimama zenyewe bila kutumia kiunganishi.
 Mfano: -Hapo zamani za kale wazee walijiheshimi; sikuhizi hawajiheshimu.
 Humpa msomaji pumziko fupi katika sentensi.
 NUKTA/ NUKTA PACHA(:)
 Alama hii hutumika
 -  kuunga sentensi mbili zinazoweza kusema zenyewe, bila kutumia kiunganishi
 -  kuunga/kuonesha vitu vilivyo katika orodha
 mfano: - Nilileta vitu hivi: wino, karatasi, embe, ndizi na nanasi.
 ALAMA YA MSHANGAO (!)
 -  Hutumika baada ya neno au usemi wa kushangaza au kushtuka
 -  Hutumika kuonesha msisitizo, kushangaa, kero n.k.
 Mfano: - Hivi ni kweli! Mwone alivyo.
 ALAMA YA KUULIZA (?)
 Huonesha hali ya kuuliza swali katika tungo/ sentensi
 Mfano: -
 -  Wanakuja saa ngapi?
 -  Wanamaana gani?
 MABANO [ ( ) ]
 Hutumika kuonesha maana ya ziada katika sentensi
 Mfano: - Nchi yangu (Tanzania) naipenda sana
 KISTARI (-)
 Hutumika kuunda maneno
 Mfano: - Ed-elfitr, Dar-es-salaam
 Hutumika badala ya nukta mbili
 Mfano: - tulipofika mbugani – tuliwaona swala wamelala – Swala dume na watoto watatu.
 - Hutumika kuonesha kama neno limekatwa kwa kuwa limefika ukingoni.
 ALAMA ZA MTAJO (“ ”)
 Hutumika kuonesha maneno yaliyosemwa na mtu mwingine katika sentensi.
 Mfano: - Nguchiro alisema “ hakika mzee Ngwale ni katili sana”
 Hutumika kubainisha maneno ya kigeni katika lugha nyingine.
 Mfano: - (“ yes” ) katika kiswahili.

UANDISHI WA INSHA
Insha ni kifungu cha habari chenye kueleza hoja au picha za mtu juu ya jambo fulani
-  Insha hugawanywa katika vifungu,  navyo ni: -
-  Insha huweza kuwa na haya moja au wakili na kila haya hubeba wazo kuu moja matumizi
-  Kuna aina kuu mbili za insha
(i)  Insha za wasifu
(ii)  Insha za hoja
INSHA

HIKI NI KIELELEZO CHA ISHA ZA HOJA NA WASIFU

INSHA ZA WASIFU

INSHA ZA HOJA
-      Insha za wasifu za kisanaa

-      Insha za wasifu zisizo za kisanaa.

-      Insha za hoja

-      Insha za kisanaa

-      Insha za hoja zisizo za kisanaa

-      Insha za wasifu

INSHA ZA HOJA
Hueleza mawazo fulani na hupanga mengine
Mifano ya vichwa vya insha vifuatavyo ni vya insha ya hoja.
-      Elimu itolewe kwa watoto wa kiume tu.
-      Shule za kutwa ni bora kuliko shule za bweni.
INSHA ZA WASIFU
Hii hueleza sifa za watu au vitu kama wanyama, milima, miti au mahali fulani: -
MAMBO YA KUZINGATIA KATIKA UANDISHI WA INSHA
  1. KICHWA CHA INSHA
   Huandikwa kwa herufi kubwa katikati juu ya insha
  Huandikwa kwa ufasaha na kwa muhtasari
  Kichwa kisizidi maneno matano(5)
  1. MWANZO WA INSHA
  Huzingatia tafsiri ya jambo linalozungumzwa, uhusiano wake na vitu vingine.
  Kwa kawaida mwanzo huzidi aya moja
  1. KIINI CHA INSHA
  Hii ni sehemu kuu ya insha huzingatia mawazo makuu ambayo hupangwa katika haya zenye mtiririko mzuri wa mawazo.
  Hueleza kwa undani juu ya jambo linalozungumzwa kwa uthibitisho.
  1. MWISHO WA INSHA
      Hutoa msisitizo kwa yaliyojadiliwa
  Huonesha muhtasari wa yaliyojadiliwa na kuandikwa pamoja na hitimisho.

   MAMBO YANAYOHITAJIKA KATIKA UTUNGAJI WA INSHA

     
1. Kichwa cha habari chenye kueleweka
  1. Kuandika kwa kufuata kanuni na taratibu za uandishi
  1. Kutumia lugha fasaha na rahisi.
  1. Andika mwisho wa insha unaowavutia wasomaji au wasikilizaji.
INSHA KUHUSU MISITU
MISITU
Mimi naitwa Ajazi Mohamed natokea kijiji cha Njoro kilichopo Moshi mkoani Kilimanjaro. Katika kijiji hicho naishi na babu pamoja na bibi alikadhalika na ndugu zangu. Kila ifikapo jumamosi mimi na ndugu zangu huwa tunakwenda kukata kuni pia kuchuma matunda kama mananasi, maembe, machungwa pia maparachichi. Misitu husaidia kwa ajili ya kivuli, mvua  pamoja na kuni. Pia misitu hiyo hiyo hutoa mbao kwa ajili ya kutengenezea vifaa vya nyumbani vikiwemo, meza, viti, makabati pamoja na vitanda. Pia mbao hutumika kujenga mapaa ya nyumba na kadhalika.
Misitu hiyohiyo hupenda kukaa wanyama wakali kama vile mbwa mwitu, nyoka na wadudu wenye sumu wakiwemo nyuki,dondola. Misitu ipo sehemu mbalimbali ikiwemo Moshi, Arusha, Songea pamoja na Singida. Misitu ni hatari sana hasa kwa watoto wadogo kwenda peke yao msituni au mwanamke kutembea peke yake jioni au usiku huwa ni hatari sana kwa sababu msituni kuna wanyama wakali sana na unaweza kukutana na majambazi.
Misitu ni muhimu kwa ajili ya mahitaji yetu ya nchi na ya nyumbani kwa ujumla pia tunasisitiza kutunza misitu, mazingira na maeneo tunayoishi.

TOFAUTI KATI YA INSHA ZA KISANAA NA ZISIZO ZA KISANAA

Insha za kisanaa
- Hizi ni Insha ambazo hutumia vipengele mbalimbali vya kifasihi katika kuwasilisha ujumbe. Mbinu hizo ni kama vile Nahau, Methali, Misemo, Tamathali za semi na mbinu nyingine za kisanaa.

Insha zisizo za kisanaa
- Hizi ni Insha ambazo hazitumii lugha ya kifasihi katika kufikisha ujumbe wake.



Post a Comment

0 Comments