Subscribe Us

header ads

fasihi kwa ujumla

FASIHI KWA UJUMLA
Fasihi:
Ni sanaa inayotumia lugha ili kufikisha ujumbe kwa jamii  iliyokusudiwa .
Ni sanaa kwa sababu huumbwa kwa lugha katika hali ya kuvutia na kuweka madoido ya kila namna ili iweze kuvutia wasomaji au wasimuliaji wake, lengo lake kuu ni kufikisha ujumbe kwa jamii.
SANAA
Ni uzuri unaojitokeza katika umbo lililosanifiwa, umbo ambalo mtu hulitumia kueleza hisia zinazomgusa kwa kutoa kielelezo chenye maana. Hivyo unaona kazi za sanaa katika nyanja mbalimbali kama vile: -
- Utarizi
- Fasihi
- Ushonaji
- Muziki
- Ususi
- Ufumaji uchoraji
    

DHIMA ZA FASIHI
(i)  Kusisimua
(ii)  Kuhifadhi na kurithisha amali za jamii
(iii) Kudumisha na kuendeleza lugha
(iv)  Kuelimisha jamii
(a)  KUSISIMUA
Hujikita zaidi katika mpangilio wa maneno lugha ya picha mandhari, tamathali au semi
Mfano: -
Ndugu yetu ametutupa mkono (amefariki)
Sentensi inajaribu kutuliza uchungu na hivyo kuleta faraja.
(b)  Kuhifadhi na kurithisha amali za jamii
Fasihi huhifadhi na kutunza mila na desturi za fani na pia huweza kurithisha mila hizo kutoka kizazi kimoja hadi kingine.
(c)  Kudumisha na kuendeleza lugha
Kwa kadri lugha inavyotumiwa na watumizi, maneno yalivyobuniwa na kuenezwa zamani, leo yanatumiwa na watunzi wa mashairi, kwaya , nyimbo n.k
(d)  Kuelimisha jamii
Fasihi hukosoa, huonya na kurekebisha jamii hueleza waziwazi wale wanaotenda kinyume na matakwa ya jamii, inabidi kukemea na kuonyana kwa kutumia methali, nahau
Mfano: - Asiyesikia la mkuu huvunjika guu
Hii inatoa tahadhari
AINA ZA FASIHI
Kuna aina mbili (2) za fasihi
(a)  Fasihi andishi
(b)  Fasihi simulizi
  1. FASIHI SIMULIZI
Ni fasihi ambayo hutumia masimulizi ya mdomo kufikisha ujumbe wake kwa jamii.
Ni fasihi ambayo ni kongwe na ilianza tangu binadamu alipoanza kuishi duniani.
FASIHI SIMULIZI INA TANZU NNE NAZO NI
(i)  Hadithi
(ii)  Semi
(iii)  Ushairi
(iv)  Maigizo

    2.  FASIHI ANDISHI
Ni fasihi ambayo hutumia maandishi ili kufikisha ujumbe kwa jamii
Fasihi andishi ina tanzu nne
(i)  Tamthilia
(ii)  Ushairi
(iii)  Ngonjera
(iv) Riwaya
TOFAUTI KATI YA FASIHI SIMULIZI NA FASIHI ANDISHI

NA

FASIHI SIMULIZI

FASIHI ANDISHI
 1

Huwasilishwa na fanani kwa njia ya masimulizi au mdomo

Huwasilishwa kwa maandishi kwa njia ya maandishi
 2

Huifadhiwa kichwani na kusambazwa na mdomo au mazungumzo

Huifadhiwa kwa maandishi na kusambazwa kwa maandishi
 3

Huruhusu mabadiliko ya papo kwa papo

Hairuhusu mabadiliko ya papohapo kazi ikishaandikwa haibadiliki hadi toleo jingine
 4

Ina tanzu nne kama vile
-      Hadithi
-      Semi
-      Sanaa za maonesho maigizo

Ina tanzu tatu kama vile
-      Ushairi
-      Tamthilia
-      Riwaya

5.

Hadhira yake ni watu wale katika jamii
-      Watoto
-      Wazee
-      Wasomi


Hadhira yake ni watu wale wanaojua kusoma na kuandika
 6

Inaumri mkubwa

Ina umri mdogo imekuwepo baada ya ugunduzi wa maandishi
 7

Ni rahisi kusahau baadhi ya vipengele

Si rahisi kusahauliwa baadhi ya vipengele kwani imehifadhiwa kwa maandishi.
 8

Muundo wake ni wa moja kwa moja

Mara nyingi muundo wake ni wa mchangamano unaruhusu urejeshi
 9

Huenda na wakati na mabadiliko ya matukio katika jamii

Haiendi na wakati kwa sababu ikishaandikwa haiwezi kubadilishwa.

TANZU ZA FASIHI SIMULIZI

Fasihi simulizi hujitokeza katika tanzu kuu nne, ambazo ni hadithi, semi, ushairi, na maigizo. Tanzu hizi zinaweza kuoneshwa katika mchoro ufuatao na vipera vyake
HADITHI
Ni tungo za fasihi simulizi zitumiazo lugha ya ujazo na maongezi ya kila siku.
Masimulizi huwa ni mafupi yaliyopangwa katika mtiririko unaokamilisha visa.
VIPERA VYA HADITHI
(i)  Ngano
(ii)  Tarihi
(iii)  Vigano
(iv)  Soga
NGANO
Hizi ni hadithi zitumiazo wahusika kama wanyama, miti na watu kuelezea au kuonya.
TARIHI
Ni hadithi ambazo husimulia kuhusu matukio ya kihistoria, matukio hayo yanaweza kuwa ya kweli au ya kubuni.
VIGANO
Ni hadithi fupi zinazoelezea makosa au uovu wa watu fulani na kueleza maadili yanayofaa. Vigano hutumia methali kama msingi wa maadili yake.
SOGA
Ni hadithi fupi za kuchekesha na kukejeli. Wahusika wa soga ni watu wa kubuni. Soga husema ukweli unaohimiza lakini ukweli huo hujenga vichekesho ili kupunguza makali.
USHAIRI
Ushairi katika fasihi simulizi ni fungu linalojumuisha tungo zote zenye kutumia mapigo ya sauti kwa utaratibu maalumu
VIPERA VYA USHAIRI
(i)   Mashairi
(ii)  Utenzi
(iii)  Nyimbo
(iv) Ngonjera
MASHAIRI
Ni tungo zenye mpangilio maalumu wa silabi na lugha ya mkato.
UTENZI
Ni tungo ndefu ya kimasimulizi au kimawaidha utenzi kutofautiana na ushauri kwa kuwa na mistari mifupimifupi isiyozidi mizani.
NYIMBO
Ni tungo zenye mpangilio maalumu wa maneno na mahadhi yaani hupenda kuimbwa na kuambatana na ala za muziki au sanaa.
NGONJERA
Zina muundo wa mashahiri ya kimapokeo na huwa katika muundo wa mazungumzo baina ya watu wawili au makundi ya watu wanaolumbana na mwishowe kufikia mwafaka/ suluhisho.
SEMI
Ni tungo za fasihi simulizi ambazo ni fupi na zenye kutumia lugha ya picha.
VIPERA VYA SEMI
(i)  Methali
(ii)  Mafumbo
(iii)  Nahau
(iv) Vitendawili
METHALI
Ni misemo ambayo hutoa hekima na busara kwa kuundwa kwa mpangilio wa pande mbili za fikra
Mfano: -
-  Kidole kimoja hakivunji chawa
-  Haba na haba hujaza kibaba
MAFUMBO
Ni kauli zinazoeleza maana waziwazi na kutumia maficho
Mfano:-
-  Hakamatiki hashikiki (moshi)
-  Uzalendo umemshinda ( umeshindwa kuvumilia)
KITENDAWILI
Ni usemi uliofumbwa hutolewa kwa hadhira, ufumbuliwe, kitendawili kufanya kazi ya kumfikisha msikilizaji.
Mfano: -
Uzi mwembamba umefunga dume (usingizi)
NAHAU
Ni kauli zilizojengwa kwa picha kwa kutumia maneno ya kawaida lakini zinatoa maana isiyo ya kawaida.
Mfano: -
-      Amepata jiko (ameoa)
-      Ana mkono mrefu (mwizi)
-      Ana mkono wa birika (mchoyo)
-      Amevaa miwani (amelewa)
MAIGIZO SANAA ZA MAONYESHO
Ni masimulizi yenye utendaji ambayo huonesha mambo yaliyotokea, yatakayotokea lengo ni kufikisha ujumbe.
VIPERA VYAKE NI:-
(i)   Michezo ya kuigiza
(ii)  Majigambo
(iii) Ngonjera
(iv)  Vichekesho
MICHEZO YA KUIGIZA
Ni maigizo marafu ya visa vinavyowakilisha maisha ya jamii fulani. Michezo mingine huafiki na mingine hulaani mambo yasiyofaa, michezo ya watoto wadogo pia huwasaidia kujifunza maadili ya jamii hiyo.
MAJIGAMBO
Ni maigizo ya kujitapa /kujigamba kutokana na kuweza kufanya jambo la kishujaa au lisilo la kawaida. Mtambaji husimulia na kutenda akionyesha jinsi alivyofanya jambo lile.
Mfano: -
Askari aliyerudi vitani,mtu aliyemuua simba n.k
NGONJERA
Ni maigizo ya kutumia mashairi, huwa kuna pande mbili unapinga na unaelewa jambo na mwisho kufikia muafaka.
VICHEKESHO
Ni maigizo mafupi ya kufurahisha hadhira
Mfano: -
-  Mizengwe
-  Original komedi
-  Vituko show
FANI NA MAUDHUI
Kazi ya fasihi lazima iwe na fani na maudhui, vipengele hivi ni sura za falsafa moja si rahisi kuzitenganisha fani imo ndani ya maudhui.
FANI
Ni umbo la nje la kazi ya fasihi
MAUDHUI
Ni jambo analosema muandishi katika kazi yake ya fasihi
VIPENGELE VYA FANI
(i)   Matumizi ya lugha
(ii)   Mtindo
(iii)   Muundo
(iv)   Mandhari au mazingira
(v)   Wahusika
(vi)  Jina la kitabu.
MATUMIZI YA LUGHA
Msanii hutoa lugha kwa mpangilio maalumu wa maneno, tamathali za semi hutumiwa kwa upekee kulingana na mahitaji ya kazi hiyo.
MTINDO
Hii ni tabia ya pekee mtunzi katika simulizi au uandishi mtindo kutofautiana hali ya mtunzi na mtunzi.
MADHARI
Ni sura ya mahali mazingira ambapo kazi ya fasihi husika
WAHUSIKA
Ni watu, miti au viumbe hai vinavyowakilisha watendaji katika kuonyesha sifa za ndani na nje.

VIPENGELE VYA MAUDHUI
Kuna vipengele (5) vya maudhui navyo ni
(i)  Dhamira
(ii)  Ujumbe
(iii) Falsafa
(iv)  Migogoro
(v) Mafunzo
DHAMIRA
Ni lengo la mtunzi wa kazi za fasihi. Mtunzi anaweza kutoa dhamira kuu na kujenga dhamira ndogondogo dhamira huweza kukosoa.
UJUMBE
Ni funzo analotoa mtunzi katika kazi ya fasihi kulingana na dhamira alizotoa
FALSAFA
Ni mawazo makuu ya mtunzi kuhusu maisha. Ni imani ya maandishi kuhusu maisha.
MIGOGORO
Ni hali ya kutoelewa na baina ya pande mbili au zaidi.
MAFUNZO
Ni mafunzo makuu ya mtunzi kuhusu maisha.wakati mwingine hadhira inaweza kupata mafunzo mabaya au mazuri kwa wahusika wakazi hiyo.
UHAKIKI WA KAZI ZA FASIHI

Maana;
Uhakiki ni kazi au kitendo cha kuchambua na kufafanua kazi ya fasihi ili kuweza kupata maadili na ujumbe uliomo katika kazi ya fasihi.

au

Uhakiki ni sayansi maalum ya kuchambua kazi ya sanaa kwa undani na kuona ubora wa kazi ya fasihi kwa kutumia vipengele vya fani na maudhui na kuangalia uwiano na uhusiano wake na jamii.

UMUHIMU WA UHAKIKI WA KAZI ZA FASIHI SIMULIZI

1. Kuchambua na kuweka wazi fumbo ambalo litapatikana na kazi ya fasihi.

2. Kuchambua na kufafanua picha za kisanii zilizotumika katika kazi ya fasihi.

3. Kumshauri mwandishi ili afanye kazi bora.

4. Kumuelekeza msomaji ili apate faida zaidi kuliko yale ambayo angeweza kuyapata bila dira ya muhakikiki (mhakiki ni mwalimu wa jamii)

5. Kuhimiza na kushirikisha fikra za kihakiki katika kazi za fasihi.

6. Kukuza kiwango cha utunzi na usomaji.

7. Kutafuta na kuweka sawa nadharia ya vitabu teule.

KUFAFANUA VIGEZO VYA UHAKIKI WA KAZI ZA FASIHI SIMULIZI.

1. Ukweli wa mambo yanayoelezwa.

2. Uhalisikaji wa watu, mazingira na matukio katika jamii.

3. Umuhimu wa kazi ya fasihi kwa jamii inayohusika lazima ufikiriwe.

UHAKIKI WA KAZI ZA FASIHI SIMULIZI KATIKA FANI.
  • Wahusika
  • Mandhari
  • Mtindo

MAUDHUI
  • Ujumbe
  • Mtindo

ZOEZI
  1. Fasihi ni nini
Fasihi ni sanaa inayotumia lugha ili kufikisha ujumbe kwa jamii fulani iliyokusudiwa
  1. Orodhesha vipera vinne (4) vya semi na mfano
(i)  Methali (kidole kimoja hakivunji chawa)
(ii)  Mafumbo ( uzalendo umemshinda)
(iii)  Nahau (amepata jiko) – Ameoa
(iv) Vitendawili (uzi mwembamba umefunga dume) – Usingizi
  1. Ainisha aina za maneno katika sentensi hii
Paka wale weusi walikuwa wanatembea ovyo barabarani
       W              TS              T                   E
  1. Taja matumizi mawili ya herufi kubwaa
(i) Hutumika kuandika jina, mahali ili kuleta maana .Mfano wa majina Asha, Ally Mfano wa mahali, Dar es salaam, Tanga n.k.
(ii) Hutumika mwanzo wa sentensi



Post a Comment

0 Comments