AINA ZA MANENO
NENO
Sio rahisi kufasiri neno, kutokana
na ukweli huo neno limeelezwa kwa namna nyingi tofautitofauti. Mathalani
wanasarufi mapokeo wanaeleza maana ya neno kwa kuangalia uhusiano wa maneno
katika tungo. Hivyo wanasema neno ni tamko lenye kubeba maana ambalo hutengwa
kwa nafasi kati ya neno na neno jingine.
Wanamuundo wanaeleza kuwa neno ni
tamko lolote lenye kuleta maana na ambalo pia laweza kuleta jibu la swali mfano
je umekula? La! kwahiyo "la" ni tamko ambalo lina hadhi ya kuwa
neno.
Kwa sarufi mapokeo maneno
yamefasiriwa kwa kuangalia maana ya maneno hayo, uhusiano wa maneno hayo na
mengine katika tungo.
Wanamuundo wanafasiri maneno na aina
zake kwa kuangalia muundo wa maneno hayo na tabia zake katika tungo pamoja na
hayo mbinu za sarufi mapokeo hutumika hapa na pale.
- Nomino
- Viwakilishi
- Vivumishi
- Vitenzi
- Vielezi
- Viunganishi
- Vihisishi
- NOMINO
Nomino ni maneno yanayotaja majina
ya watu, wanyama, mahali, vitu n.k. Tabia zake kimuundo ni maneno yanayochukua
viambishi, ngeli ambavyo pia vinaonyesha idadi. Aidha Nomino ni maneno makuu
yanayotawala kirai nomino, mfano jua,Seif, Morogoro n.k.
AINA ZA NOMINO
(a) Nomino za pekee
Ni maneno yanayotaja watu, mahali,
maumbile mbalimbali ya kijiografia n.k. angalau maneno haya yanapoandikwa
huanzia na herufi kubwa mfano: Nyerere, Ali, Singida, Nile n.k.
(b)Nomino za kawaida
Ni maneno yanayotaja vitu vyenye
tabia za kifaradhi (universal) mfano: mtoto, mtu, nyumba, baba n.k.
(c) Nomino za jumla
Nomino zinazotaja vitu katika uwingi
wake mfano jeshi, mchunga, kundi, jamii n.k
(d)Nomino dhahania
Nomino zinazotaja vitu visivyoweza
kuonekana au kushikika aghalabu vitu hivi huwa vya kifikra au kusadikika mfano,
njaa, furaha, upepo zimwi n.k
- VIWAKILISHI
Ni maneno ambayo hutumika badala ya
nomino ambayo yanatabia zilezile za kinomino mfano kutawala kirai nomino na
kuchukua viambishi ngeli mfano, wewe, sisi n.k.
AINA ZA VIWAKILISHI
(a) Viwakilishi nafsi – hivi
ni viwakilishi ambavyo hubainisha nafsi za wazungumzaji
(i) Viwakilishi nafsi huru ni maneno
kamili mfano: -
UMOJA WINGI
Nafsi
I Mimi
sisi –
Mzungumzaji
Nafsi II
wewe
ninyi/ nyinyi – msikilizaji
Nafsi III yeye
wao – mzungumzaji
(ii) Viwakilishi nafsi
viambata – hivi vipo katika umbo la mofimu na huambatanishwa na vitenzi mfano:
-
UMOJA
WINGI
Nafsi
I
Ninakuja
Tunakuja
Nafsi II
Unakuja
mnakuja
Nafsi II
Anakuja
wanakuja
(iii) Viwakilishi vya kumiliki
Hubainisha dhana ya kumiliki
Mfano: angu, enu, ako, ake n.k
(iv) Viwakilishi vya kuuliza
Hivi hudokeza maswali
Mfano: kipi, gani, epi n.k
(v) Viwakilishi vya kuonesha
Mfano: huyu, hawa, zile, kile, hiki
n.k
(vi) Viwakilishi vya
msisitizo;- ndi - na - amba- - mfano ndiye, ndiwe, ambaye, ambalo n.k
- Viwakilishi
vya kumiliki, kuuliza na kuonesha hutumika kama vivumishi iwapo vitaambatana na
nomino
Mfano:
o Mtoto wangu sijamuona
o Mtoto wako amefika
wangu hajaonekana bado
Wakati mwingine kiwakilishi huweza
kuwa nomino, kiwakilishi au kitenzi
Mfano: -
o Kiti kizuri
kimevunjika
o Kizuri kimevunjika
o Anacheza vizuri
- VIVUMISHI (V)
Kimapokeo vivumishi ni maneno ambayo
yanaambatana na nomino au viwakilishi yakitoa taarifa juu ya nomino au
viwakilishi hivyo.
Katika sarufi muundo vivumishi ni maneno
yanayochukua viambishi ngeli kama ilivyo katika nomino na aidha ni maneno
yanayotawala kirai vumishi.
Mfano:-
Mkubwa, kubwa,kikubwa. Viambishi
awali ni viambishi ngeli
AINA ZA VIVUMISHI
Muainisho wa vivumishi hutegemea
zaidi dhima ya kisemantiki katika tungo. Kwa mfano kisemantiki vivumishi
vyaweza kuwa vyakueleza namna au jinsi idadi, kuuliza n.k.
(i) Vivumishi vya sifa
Kwa kiasi kikubwa hivi hueleza namna
au jinsi ya nomino au kiwakilishi mfano: -
(a) Vivumishi halisi: - Hivi
havichukui viambishi ngeli mfano: hodari
(b) Vivumishi visivyo halisi:
- mfano hivi ni vile vinavyochukua viambishi ngeli – pole, -kubwa, ...... n.k
(ii) Vivumishi vya kuuliza
Ni vivumishi vinavyodokeza swali
mfano:
- Mtoto yupi?
- Nyumba gani?
(iii) Vivumishi vya kumiliki
Hivi hujenga dhana ya umilikaji
mfano:
- Kiti changu
- Kazi zetu
- Tabia yako
(iv) Vivumishi vya kuonesha
Hivi hudokeza umbali au ukaribu wa
nomino mfano:
- Nyumba hii
- Watoto wale
(v) Vivumishi vya idadi
Ni vivumishi vinavyodokeza idadi
katika dhana ya umoja au wingi mfano:
- Watoto wawili
- Watu wengi
- Maji kidogo
(vi) Vivumishi vya jina kwa jina
Vivumishi vya aina hii ni nomino
ambazo huwa na dhima ya kuvumisha nomino au kiwakilishi mfano:
- Mwalimu Zakia
- Baba Juma
(vii) Vivumishi vya –A-
unganifu
Ni vivumishi vinavyojenga dhana ya
kimilikisho ambayo hujengwa na j=kiambata –a- kinachochukua kiambishi ngeli
kadiri ya nomino milikishwa mfano:
- Nyumba ya baba
- Kitenge cha mama
(viii) Vivumishi vya –enye-,
-enyewe- mfano:
- Mtoto mwenye
- Nyumba yenye
- Mtoto mwenyewe
- Nyumba yenyewe
(ix) Vivumishi vya o-te-
Mfano: -
- Nyumba yoyote
- Kiwanja chochote
(x) Vivumishi vya– ingine
–engine
Mfano:
- Kiti kingine
- Watu wengine
- VITENZI
Kimapokeo vitenzi ni maneno
yanayoeleza jambo linalotendwa na nomino au hali ya nomino mfano:
(a) Juma anacheza mchezo
(b) Juma ni mgonjwa
Kimuundo vitenzi ni maneno
yanayounda kirai tenzi na aidha huchukua vipatanisho vya kisanifu vilevile vina
uwezo wa kujenga dhana mbalimbali mfano: njeo, haki tofauti, kauli tofauti
tofauti n.k
Mfano :-
- Mtoto anacheza
- Watoto wanacheza
AINA YA VITENZI
Katika sarufi mapokeo vitenzi ni vya
aina tatu,
(i) vitenzi vikuu (T)
(ii) vitenzi visaidizi (TS)
(iii) vitenzi vishirikishi (t)
kwa sarufi muundo vitenzi ni vya
aina mbili
(a) vitenzi halisi
Hivi vina sifa kamili ya kileksika
vinasimama peke yake na kuunda KT yaani kirai tenzi (T), mfano: mtoto kaja ,
wale wanalia
T
T
(b) Vitenzi vipungufu: -
(visivyo halisi)
Hivi ni vitenzi ambavyo havina hadhi
kubwa kama vitenzi halisi.
Kimapokeo vinaitwa vitenzi visaidizi
kazi yake kubwa ni kusaidia vitenzi vikuu kujenga dhana au maana ya ziada
kuhusiana na kitenzi kikuu
mfano:- Ndege alikuwa anacheza
Ts
T
VITENZI VISHIRIKISHI (t)
Hivi ni vitenzi vipungufu na dhima
yake ni kuonesha uhusiano baina ya nomino au kiwakilishi na maneno mengine
katika tungo mfano: nomino, kiwakilishi, kivumishi au kitenzi.
Mfano: -
Juma ni mchezaji
t
juma ndiye wewe
t
Mtoto alikuwa hodari
t
Mtoto yumo ndani
t
AINA ZA VITENZI VISHIRIKISHI
Vitenzi vishirikishi ni vya aina
tofautitofauti kutegemea dhana inayobebwa na vitenzi hivyo kisemantiki
(a) Vitenzi vya KUWA
Mfano: hali yakinishi
kanushi
(i)
Alikuwa
hakuwa
(ii) Ni
si
(iii)
Atakuwa
hatakuwa
(b) Vitenzi vya kuwa NA
Ni vitenzi vinavyojenga dhana ya
kumiliki mfano
(i) Mama alikuwa na nyumba
(ii) Mama ana nyumba
(iii) Mama atakuwa na nyumba
(c) Vitenzi vya mofimu – PO- ,
- MO -, - KO-.
Mfano:-
(i) Simba yupo ndani
(ii) Mtoto yumo ndani
(iii) Mtoto yuko nje
(d) Vitenzi vya msisitizo NDI
Mfano: -
(i) Huyu ndiye Juma
Huyu siye
(ii) Wewe ndiwe Juma
sisi ndio wenyewe
(e) Vitenzi vya msisitizo AMBA
Mfano:
(i) Huyu ambaye yupo
(ii) Hawa ambao wapo
- VIELEZI
Vielezi ni maneno ambayo ni vigumu
kuyafasihi moja kwa moja isipokuwa yanafasihika kutokana na tabia zake na
jukumu la kimantiki katika TUNGO.
Mfano: - kuna vielezi vinavyoeleza
juu ya kivumishi, vingine juu ya vitenzi na kielezi kingenecho.
(a) Mtoto mwema sana
(b) Mtoto anakuwa taratibu
(c) Mtoto anakuwa taratibu mno
AINA ZA VIELEZI
Pamoja na kwamba vielezi vina tabia
ya kuhamahama, kudondosheka katika tungo pia vinajibu maswali kadhaa katika
tungo. Kutokana na maswali yanayojibiwa na vielezi ni vya aina nne.Mfano: -
(a) Vielezi vya namna au jinsi
Mfano: mtoto anatembea
polepole
Anaongea kinyumenyume
(b) Vielezi vya mahali (wapi)
Mfano: - Mbwa alibweka magengeni
(c) Vielezi vya idadi au kiasi
(mara ngapi kwa idadi gani)
Mfano: - wanacheza mara kwa mara
(d) Vielezi vya wakati (lini)
Alionekana juzi
Pamoja na idadi hii ya vielezi kuna
vielezi vya ziada
Mfano:- vielezi vya kasoro au
upungufu, vya sababu, vya hali ya masharti n.k
- KIUNGANISHI (U)
Haya ni maneno yanayojenga dhana ya
uunganikaji baina ya neno na neno, kirai na kirai, kishazi na kishazi, sentensi
na sentensi
Mfano:- na, ila, bali, pia, ama, au,
pamoja na alama ya koma.
- VIHISISHI (H)
Haya ni maneno yanayodokeza vionjo
vya moyo, yanaponukuliwa yanaambatana na alama ya mshangao, yala! Oye! Oh!
Masalale! Lahaulaa, Alaa!!
MATUMIZI YA KAMUSI
Kamusi;- Ni kitabu cha maneno yaliyopangwa kwa utaratibu wa kialfabeti na kutolewa maana na maelezo mengine. Kitabu hiki huwa na idadi kubwa ya maneno kutoka katika lugha husika, na maneno hayo hutolewa maana na maelezo kwa lugha hiyohiyo au kwa lugha nyingine.
MUUNDO WA KAMUSI
Kamusi yoyote ile imegawanyika katika sehemu tatu nazo ni;-
a) Mwongozo wa msomaji (Utangulizi wa kamusi)
b) Vifupisho na matumizi ya alama
c) Kamusi yenyewe (matiri ya kamusi)
a) Mwongozo wa msomaji
Ni usuli ambao unalenga kumuelekeza mtumiaji wa kamusi ili aweze kutumia kamusi hiyo bila kupata usumbufu. Muongozo wa msomaji huhusika na mambo yafuatayo;-
i) Taarifa zilizoingizwa kam vile;
- Vidalizo.
- Vibadala vya vidalizo.
ii) Kategoria ya maneno
- Nomino
- Vitenzi
- Vielezi
- Vivumishi
- Umoja na wingi n.k
iii) Maneno na utumizi wa maneno
mfano;- Nomino (sarufi)
- Elementi (kemia)
iv) Mifano ya matumizi
v) Lugha kienzo.
b) Ufupisho wa matumizi ya alama
Ni muhimu kwa mtumiaji wa kamusi kupata taarifa zinazohusu matumizi mbalimbali ya vifupisho , tarakimu, herufi na maana.
Mfano;- agh - aghalabu
ele - elekeza
fiz - fizikia
Kb - kibaharia
Kd - kidini
Kh - kihusishi
K.v - kamavile
Kv - kivumishi
Mt - methali
nh - nahau
n.k - Na kadhalika
c) Kamusi yenyewe
Hii ni sehemu ambayo inakuwa na orodha ya maneno mbalimbali yenye maana na ufafanuzi wa neno husika. Sehemu hii ndio kiini cha kamusi.
UFAFANUZI WA ISTILAHI MUHIMU KATIKA MADA HII YA UTUMIZI WA KAMUSI
Ni vema kufahamu istilahi kuu katika kujadili mada hii. Istilahi hizo ni hizi zifuatazo;
i) Kidahizo
ii) Kitomeo
iii) Lugha kienzo
i) KIDAHIZO
Kidahizo ni neno lilioingizwa katika kamusi ili lipatiwe maana na ufafanuzi mwingine wa kisarufi (kimatamshi, kimuundo) na kimatumizi. Vidahizo huandikwa kwa kukolezwa wino.
Mfano;- abee! bee! (kwa wanawake ) neno la kuitika wanapoitwa.
Mpangilio wa vidahizo
Kutokana na tofauti za kimuundo katika aina moja ya neno na aina nyingineya neno kikategoria, vidahizo huwekewa utaratibu maalum katika kuingiza vidahizo hivyo. Jambo la msingi kuelewa ni kwamba ,vidahizo hupangwa kwa kufuata utaratibu wa kialfabeti.
ii) KITOMEO
Kitomeo ni kidahizo na maelezo yake yote. Au kitomeo ni neno lililoingizwa katika kamusi kama kidahizo pamoja na taarifa zake zote. Kwa mfano;-
Kitomeo cha 1. Maalimu - Ni mtu mwenye elimu kubwa ya dini ya kiislamu.
Kitomeo cha 2. aathari - Ni masalio ya vitu na utamaduni wa watu fulani.
Kitomeo cha 3. abaa! - Neno la kumwita rafiki, alaa! Aisee!
Kitomeo cha 4. abadani! Ni neno linalosisitiza jambo la ufupi, ufasaha, utoshelevu na uwazi . Mtindo huu hutumia alama zinazofupisha maelezo marefu au fasihi mbalimbali.
iii) LUGHA KIENZO
Ni mtindo unaotumika kutolea fasihi za vidahizo katika kamusi kwa ufupi, ufasaha, utoshelevu na uwazi. Mtindo huu hutumia alama zinazofupisha maelezo marefu au fasihi mbalimbali.
MATUMIZI YA KAMUSI
Kamusi;- Ni kitabu cha maneno yaliyopangwa kwa utaratibu wa kialfabeti na kutolewa maana na maelezo mengine. Kitabu hiki huwa na idadi kubwa ya maneno kutoka katika lugha husika, na maneno hayo hutolewa maana na maelezo kwa lugha hiyohiyo au kwa lugha nyingine.
MUUNDO WA KAMUSI
Kamusi yoyote ile imegawanyika katika sehemu tatu nazo ni;-
a) Mwongozo wa msomaji (Utangulizi wa kamusi)
b) Vifupisho na matumizi ya alama
c) Kamusi yenyewe (matiri ya kamusi)
a) Mwongozo wa msomaji
Ni usuli ambao unalenga kumuelekeza mtumiaji wa kamusi ili aweze kutumia kamusi hiyo bila kupata usumbufu. Muongozo wa msomaji huhusika na mambo yafuatayo;-
i) Taarifa zilizoingizwa kam vile;
- Vidalizo.
- Vibadala vya vidalizo.
ii) Kategoria ya maneno
- Nomino
- Vitenzi
- Vielezi
- Vivumishi
- Umoja na wingi n.k
iii) Maneno na utumizi wa maneno
mfano;- Nomino (sarufi)
- Elementi (kemia)
iv) Mifano ya matumizi
v) Lugha kienzo.
b) Ufupisho wa matumizi ya alama
Ni muhimu kwa mtumiaji wa kamusi kupata taarifa zinazohusu matumizi mbalimbali ya vifupisho , tarakimu, herufi na maana.
Mfano;- agh - aghalabu
ele - elekeza
fiz - fizikia
Kb - kibaharia
Kd - kidini
Kh - kihusishi
K.v - kamavile
Kv - kivumishi
Mt - methali
nh - nahau
n.k - Na kadhalika
c) Kamusi yenyewe
Hii ni sehemu ambayo inakuwa na orodha ya maneno mbalimbali yenye maana na ufafanuzi wa neno husika. Sehemu hii ndio kiini cha kamusi.
UFAFANUZI WA ISTILAHI MUHIMU KATIKA MADA HII YA UTUMIZI WA KAMUSI
Ni vema kufahamu istilahi kuu katika kujadili mada hii. Istilahi hizo ni hizi zifuatazo;
i) Kidahizo
ii) Kitomeo
iii) Lugha kienzo
i) KIDAHIZO
Kidahizo ni neno lilioingizwa katika kamusi ili lipatiwe maana na ufafanuzi mwingine wa kisarufi (kimatamshi, kimuundo) na kimatumizi. Vidahizo huandikwa kwa kukolezwa wino.
Mfano;- abee! bee! (kwa wanawake ) neno la kuitika wanapoitwa.
Mpangilio wa vidahizo
Kutokana na tofauti za kimuundo katika aina moja ya neno na aina nyingineya neno kikategoria, vidahizo huwekewa utaratibu maalum katika kuingiza vidahizo hivyo. Jambo la msingi kuelewa ni kwamba ,vidahizo hupangwa kwa kufuata utaratibu wa kialfabeti.
ii) KITOMEO
Kitomeo ni kidahizo na maelezo yake yote. Au kitomeo ni neno lililoingizwa katika kamusi kama kidahizo pamoja na taarifa zake zote. Kwa mfano;-
Kitomeo cha 1. Maalimu - Ni mtu mwenye elimu kubwa ya dini ya kiislamu.
Kitomeo cha 2. aathari - Ni masalio ya vitu na utamaduni wa watu fulani.
Kitomeo cha 3. abaa! - Neno la kumwita rafiki, alaa! Aisee!
Kitomeo cha 4. abadani! Ni neno linalosisitiza jambo la ufupi, ufasaha, utoshelevu na uwazi . Mtindo huu hutumia alama zinazofupisha maelezo marefu au fasihi mbalimbali.
iii) LUGHA KIENZO
Ni mtindo unaotumika kutolea fasihi za vidahizo katika kamusi kwa ufupi, ufasaha, utoshelevu na uwazi. Mtindo huu hutumia alama zinazofupisha maelezo marefu au fasihi mbalimbali.
0 Comments