Njia nane za kuboresha uwezo wa ubongo
wako
Umeshajipata katika hali ambapo unajaribu bila mafanikio kukumbuka
jina la mtu au kitu fulani au mahala fulani lakini huwezi kukumbuka kabisa?
Mara nyingi tunaambiwa kuwa uwezo wa kukumbuka unapungua wakati
mtu anazidi kuwa mzee.
Lakini kuna matumaini kuwa kuna njia za kuboresha ubongo wetu.
Kwa hivyo kama unataka kuboresha uwezo wa ubongo wako basi kuwa
tayari kufanya mambo haya.
1. Mazoezi hufanya
ubongo wako kuwa mkubwa
Ni kweli ubongo wetu huwa mkubwa wakati tunafanya mazoezi.
Mazoezi huchangia ubongo kuwa na mawasiliano mazuri na pia huchangia
seli zaidi kukua.
Kama unafanyia mazoezi yako nje basi inakuwa bora kwa sababu
utakuwa na manufaa zaidi ya kupata vitamini D
Fanyia mazoezi katika mazingira mapya na njia mpya za kufanya
mambo mengine.
2. Kariri vitu
ukiendelea na shughuli zingine.
Hii ni mbinu ambayo pia imetumiwa na wacheza filamu: kama
unajaribu kukariri maneno fulani au kujaribu kujifunza kitu huku ukitembea
tembea, unaweza kushika kwa njia rahisi kile unachokariri.
Ikiwa wakati mwingine utakuwa labda na hotuba ya kukariri, mbona
usitembetembe au ucheze densi kukusaidia kushika kwa njia rahi kile
unachokifanya.
3. Kula chakula
kinachosaidia kukua kwa ubongo.
Karibu asilimia 20 ya sukari au chakula cha kutupa nguvu
unachokula kinaelekea kwa ubongo, na kuufanya ubongo kutegemea sana sukari.
Ikiwa viwango vya sukari haviwezi kudhibitiwa akili yako itahisi
kuchanganyikiwa. Ukila chakula unachokipenda hutoa kemikali inayojulikana kama dopamine
kwa eneo fulani la ubongo na ndio maana unahisi vizuri ukila chakula hicho.
Seli za ubongo hujengwa kwa mafuta, kwa hivyo ni muhimu kutotoa
mafuta kutoka kwa chakula chako. Mafuta kutoka kwa njugu, nafaka , parachichi
na samaki ni muhimu kwa afya ya ubongo.
4. Kupumzika.
Misongo mingine ya
mawazo ni muhimu kwa sabubu inatuwezesha kuchukua hatua za haraka wakati
dharura: huchangia homoni kwa jina cortisol na wakati ikipasuka hutuwezesha
kupata nguvu na kufanya jamba kwa umakini.
Lakini msongo wa muda
mrefu huathiri sana ubongo.
Kwa hivyo ni muhimiu
kujua kuwa tunastahili kupumzika mara moja kwa wakati fulani kuwezesha pia
ubongo kupumzika.
5. Tafuta njia zingine
za kujipa changamoto.
Njia muhimu ya kuboresha ubongo wako ni kuuoa changamoto kwa
kujifunza kitu kipya kabisa.
Shughuli kwa mfano kujifunza kuchora au kujifunza lugha mpya
huchangia ubongo kuboreka zaidi.
Unaweza pia kucheza michezo ya mitandaoni dhidi ya marafiki au
watu wa familia.
6.
Sikiliza Muziki
Ushahidi unaonyesha kuwa muziki huboresha ubongo kwa njia ya
kipekee
Wakati ukingalia ubongo wa mtu ambaye anasikiliza muziki au
anayecheza muziki ni kuwa ubongo wote hushiriki.
Jiunge na kikundi na waimbaji au lipa tiketi kuhudhuria tamasha
la bendi unayoipenda.
7.
Somea mtihani kitandani
Kama utajifunza kitu kipta wakati wa mchana, huwa kunatokea
mawasiliano kati ya seli moja ya ubongo na nyingine
Unapolala, mawasiliano huwa dhabiti na huwa unakumbukakile
umejifunza.
Kwa hivyo kulala ni kitu muhimu katika kujikumbusha kile
umesoma.
Ikiw unampa mtu kitu cha kujifunza kabla hajalala, watakikumbuka
wanapoamka asubuhi kuliko kumpa mtu kitu cha kukariri mapema asubuhi.
Ikiwa unasomea mtihani, jaribu kupitia maswali na majibu
kichwani mwako wakati unakaribia kulala.
8. Amka vizuri
Sote tunaju kuwa
kulala ni kitu muhimu, chini ya saa tano za kulala hautafikiria vizuri, huku
kulala zaidi ya saa kumi utahisi umechoka.
Lakini jambo ku
litakalokuwezeha kufanya vyema siku nzima ni jinsi utaamka.
Lala kwenye chumba
chennye giza na amka ukiongeza mwangaza taratibu.
Mwangaza huu hupitia
kwenye macho yaliyofungwa na kuujulisha ubongo ili kuamsha homoni inayoitwa
cortisol.
Kiwango cha homoni ya
cortisol mwilini mwako wakati unapoamka huathiri jinsi ubongo wako utafanya
kazi siku hiyo.
1 Comments
Kiukweli nimefaidika ahsante
ReplyDelete